Dodoma Stars Musical Club...Taarab ndani ya Dodoma









Kundi la Taarab la Dodoma Stars Music Club limo katika mazoezi makali ya kujifua ilikurudisha heshima ya kundi hili kongwe. Niliwakuta wanamuziki wa kundi hili wakiwa katika mazoezi makali kutokana na waimbaji wengi kuwa wapya na bado ni wachanga katika fani hii. Kundi hili limekuwa chimbuko la wanamuziki wengi wa Taarab akiwemo Ally Star, ambaye alipata jina la Star kutokana na kuweza kuokua jahazi kwa kupiga kinanda na kuimba peke yake akisaidiwa  na mke wa mzee Jela, baada ya wanamuziki wote wa kundi hili kuhama ghafla wakati kikundi kililazimika kupiga katika harusi fulani

Comments