Mbunifu wa amplifaya za Marshall aaga dunia

Kwa wapiga magitaa wengi duniani hasa wa muziki wa rumba na hata rock, hakuna amplifaya ilikuwa ikizidi ile ya aina ya Marshall. Amplifaya hizi zilikuwa na sauti bora, zilikuwa imara, na binafsi nilipendelea zaidi zile amplifaya zilizokuwa zinatumia valve kabla ya hizi za sasa zinazotumia IC, zilikuwa na aina ya pekee ya uzito wa sauti. Lakini ni jambo la kusikitisha mwanzilishi wa utengenezaji wa amplifaya hizi amefariki na kuacha urithi wa kazi yake dunia nzima. Mungu amlaze pema Jim Marshal aliyepewa jina "Father of loud'- Baba wa kelele kwa kuwa amplifaya zake zilikuwa maarufu sana kwa wanamuziki wakubwa wengi na zilitegemewa sana katika matamasha makubwa duniani. Soma hapa habari zake zaidi Jim Marshal

Comments