Rebecca Malope kuwepo katika Tamasha la Muziki wa Injili


Rebecca Malope kuwepo katika Tamasha la Muziki wa Injili April 8 2012 Uwanja wa Taifa. Muimbaji huyu mahiri kutoka Afrika Ya Kusini  ana historia ya muziki inayoanzia 1986. Wakati huo Rebecca akiwa na umri wa miaka 21 na akiwa na dada yake Cynthia waliondoka kwao Lekazi na kusafiri kwa shida hadi mji wa Evaton kiasi cha kilomita 400 na baadae kuingia jiji la Johannesburg wakiwa na nia moja tu kuwa wanamuziki. Rebecca amekwisha toa album 32 na pia kupata tuzo ya Kora kwa muziki wa Gospel.

Comments