Onyesho la muziki la katika DICOTA Convention 2011 Washington DC

Andy Swebe na King Kiki wakiwa kwenye microphone
Wanamuziki watatu walisafiritoka Dar es Salaam kwenda Washington DC ili kwenda kushiriki katika kutoa burudani katika mkutano wa DICOTA Convention 2011. King Kiki, Andy Swebe na Maneno Uvuruge walisindikizana na kuweza kuungana na wana muziki kama Ngouma Lokito na Lokassa Ya Mbongo na kuporomosha nyimbo nyingi za zamani kuanzia Kitambaa Cheupe hadi Rangi ya Chungwa na kuwafurahisha sana waliohudhuria

Comments