Kanku Kelly aelekea Thailand


Mwanamuziki mkongwe wa siku nyingi Kanku Kelly alilazimika kuondoka kabla ya kushiriki usiku wa Sauti za Kale baada ya kulazimika yeye na bendi yake Kilimanjaro Connection kulazimika kuwahi mkataba ambao aliupata katika nchi ya Thailand. Kanku pia amesindikizana na mwanamuziki mwingine mkongwe Mafumu Bilali ambaye ilikubalika japo ashiriki katika onyesho la Sauti za Kale na kesho yake kupanda ndege kumfuata Kanku Kelly. Wanamuziki wote wawili licha ya kushiriki kikamilifu  na kutoa mchango mkubwa katika kundi la wanamuziki wakongwe pia walishiriki katika kurekodi nyimbo tatu ambazo kundi hili lilirekodi

Comments