Carola Kinasha Sweet Eazy Ijumaa hii


Mwanamuziki muimbaji mahiri Carola Kinasha atakuwa katika ukumbi wa Sweet Eazy ( Oysterbay, Dar es Salaam), wiki hii siku ya Ijumaa 17 June 2011. Carola ambaye ni mwanamuziki wa miaka mingi aliyewahi kupitia vikundi kama Watafiti, Shada Group na bendi ya kimataifa iliyoluwa na wapigaji akinamama watupu Women Voices ambayo ilifanywa maonyesho katika nchi mballimbali duniani, ni mwimbaji ambaye ni burudani kumsikiliza. Usikose onyesho hili. Kwa maelezo zaidi piga simu +255 777461911 Kwame Mchauru. Au bonyeza hapa

Comments