Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo kukutana wasanii


Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dr. Emmanuel Nchimbi (Mb), atakutana na wasanii katika ukumbi wa BASATA kuanzia tarehe 17 Mei na tarehe 18 Mei, 2011. Waziri ataongea na wasanii kwa utaratibu ufuatao:-
 17/05/2011 (Jumanne) Saa 4:00 asubuhi

Wasanii Wote wa Sanaa za Muziki
18/05/2011 (Jumatano) Saa 4:00 asubuhi
Wasanii Wote wa Sanaa za Ufundi,Filamu na Maonyesho
Izingatiwe kwamba Waziri ataongea na wasanii wa muziki wa aina zote wakiwemo wa Kizazi kipya,Bendi,Disco, Asili,Taarab na kadhalika katika siku ya kwanza.Katika siku ya pili yaani Tarehe 18/05/2011 ataongea na wasanii wa Sanaa za Filamu,Maonyesho na Ufundi pekee. Wasanii Wote mnaombwa kujitokeza kwa wingi.
Lengo kuu la mikutano hii kati ya Waziri na Wasanii ni kuongelea maendeleo ya fani za sanaa.

Ghonche Materego

KATIBU MTENDAJI

Comments