Kings Modern Taarab

 Leo nilikaribishwa kwenye kikao cha kundi jipya la Taarab, Kings Modern Taarab, Jina hilo linatokana na mahala wanapofanyia mazoezi, Kings bar Mburahati. Kundi hilo lenye wasanii 18, liko chini ya Kijoka, mtunzi na muimbaji wa siku nyingi. Tayari wamekwisha rekodi album mbili ambazo hawajazizindua na hivyo walikuwa katika vikao vya kupanga ratiba za uzinduzi. Nyimbo ambazo tayari ziko redioni ni Mchumia juani, na zilizo katika video kwenye TV ni Roho Mbaya, Masharoharo, na nyingine mbili


Kijoka

Comments