Haya wasanii chipukizi jitokezeni mtumie nafasi hii

Wanamuziki wengi maarufu duniani wametokana na kupatikana katika maonyesho au mashindano ya aina kama hii.Nashauri wanaoweza kujitokeza wajitokeze tuwaone.
Fomu za kuwapata washiriki watakaounda kundi la muziki wa Bongo Fleva kupitia Shindano la Jenga Nchi Yako, zimeanza kutolewa katika Ofisi za Kampuni ya Global Publishers Bamaga-Mwenge, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mratibu wa shindano hilo, Richard Manyota(Pichani), mchakato ulianza wiki hii kwa kila mshiriki kujipatia fomu hiyo kwa shilingi 3,000, walengwa wakiwa ni wakazi wa Jiji la Dar es Salaam pekee na wasanii watakaofanikiwa kuunda kundi hilo watarekodi wimbo mmoja bure.

Mratibu huyo aliwataka wakazi wa Dar es Salaam na vitongoji vyake wajitokeze kwa wingi kuchukua fomu hizo kwa sababu zilizopo ni chache.

Comments