Cassava Band

Nilikuwa napita karibu na Maryland Bar Mwenge, nikasikia wimbo Kadiri kansimba ukipigwa na kuimbwa vizuri, sikuwa na ujanja ilikuwa lazima nikaione bendi inayopiga vizuri namna hiyo, nilipata mshangao. Nusu ya wanamuziki nawafahamu na sijaonana nao siku nyingi. Kwenye drum alikuweko Kejeli Mfaume, huyu tulikuwa nae Tancut Almasi na ndie aliyerekodi nyimbo nyingi za awamu ya kwanza ya Tancut Alimasi na sasa alikuwa pia anaimba kwa sauti tamu, kweli miaka inapita Kejeli hakuwa anaimba enzi hizo. Mshangao wa pili ni kumwona Sakul kwenye solo, mara ya mwisho nilimkuta Sakul Tabora Hotel akiwa na bendi moja huko, Sakul ana ulemavu wa macho haoni lakini kwenye solo wacha kabisa. Pembeni yake kwenye gitaa la rythm alikuweko Kienze, huyu nilifahamiana nae mara ya kwanza mwaka 1995, wakati huo akiwa katika kundi la SBB- Seven Blind Beats, nae pia ana ulemavu wa macho haoni, lakini kwa rythm gitaa kaa mbali. Wakali hawa watatu wakiwa pamoja lazima kieleweke. Nikajikuta nachukua gitaa na tukapiga Masafa Marefu, tukapiga Mtaulage loh nilirudishwa mbaali. Thanks guys

Kejeli Mfaume

Kienze-Rythm Gitaa

Sakul-Solo gitaa


Ally


Ally Konde

Juma




Comments