MAHAKAMA YATUPILIA MBALI MAOMBI YA HAMISA MABETO DHIDI YA DIAMOND PLATNUMZ

Hakimu Devotha Kisoka wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo ametupilia mbali kesi iliyofunguliwa na Hamisa Mabeto dhidi ya mwimbaji  mashuhuri  Diamond Platnumz. Hamisa alifungua kesi ambayo pamoja na mambo mengine alikuwa akiomba matunzo ya mtoto waliyezaa pamoja na muimbaji huyo. Hamisa alikuwa akiiomba mahakama imuamuru muimbaji huyo pamoja na mambo mengine atoe matunzo ya milioni tano kwa ajili ya mtoto.

Katika hati ya majibu kinzani, Diamond alieleza kuwa maombi ya matunzo ya mtoto ya shilingi milioni tano kwa mwezi ni makubwa mno hawezi kuyamudu.

Comments