Mshindi wa Singeli Michano ya EFM Mwanza apatikana

>
Watanzania jana waliadhimisha kumbukizi ya miaka 18 tangu kufariki dunia kwa mwasisi wa taifa la Tanzania, Hayati Mwl.Julius Kambarage Nyerere aliyefariki dunia Oktoba 14,1999 akiwa nchini Uingereza kwa ajili ya matibabu.

Lakini wakati huo huo katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza, uliofunguliwa na Mwl.Nyerere mwaka 03.02.1980 kulifanyika tamasha la Mziki Mnene lililoandaliwa na EFM & ETV za Dar es salaam.

Katika tamasha hilo kuna matukio muhimu yaliyofanyika ambapo asubuhi ilianza na mazoezi ya viuongo (Jogging) pamoja na kumsaka mkali wa muziki wa Singeli yaani "Singeli Michano" . Mchana kulikuwa na mchezo wa soka baina ya kikosi cha EFM&ETV na timu ya Mwanza Veteran na jioni hadi kuchee ilifanyika burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.

BMG imekusogezea mshindi wa Singeli Michano Mwanza #Live kutoka uwanja wa CCM Kirumba ambako tamasha hilo lililodhaminiwa na wadhamini kadhaa ikiwemo Biko, Cocacola na JB Fairmont Hotel.
 
Habari imeandaliwa na BMG Habari, Pamoja Daima!

Comments