WANAMUZIKI KARIBUNI KUSHIRIKI TAMASHA LA MUZIKI LA KARIBU MUSIC FESTIVAL 2017


The Karibu Music Festival (KMF) yaja tena kwa mara ya nne katika mji wa Bagamoyo. Mwaka huu Tamasha hilo litakuwepo kuanzia Ijumaa tarehe 3 hadi Jumapili tarehe 5 Novemba.. Mwaka huu kunategemewa kuweko kwa wanamuziki kutoka  nchi mbalimbali za Afrika, Ulaya.Amerika na Asia, ambao watafanya maonyesho na pia kuendesha warsha mbalimbali. Wanaotaka kushiriki maombi yanapokelewa mpaka tarehe 31 mwezi Agosti 2017, wanaotaka kushiriki wanashauriwa kuwahi kutuma maombi. Wasanii kutoka Tanzania wanatapata posho kiasi , wakati wasanii kutoka nje watajitegemea kwa usafiri wa kuja mpaka Dar na huku watapewa malaziusafiri wa ndani na posho.Maswali yote kuhusu tamasha hili yatumwe info@karibumusic.org

KMF inatayarishwa na  Karibu Cultural Promotions Organisation kwa ushirikiano na  Legendary Music. Watayarishaji wanalenga katika kutoa mchango katika kukuza muziki wa Afrika na kujenga mahusiano kati ya washiriki. Tamasha litafanyika katika viwanja vyenye ukubwa wa hekta 200 vilivyo eneo la chuo cha sanaa cha TASUBA Tamasha ni wazi kwa kila aina ya muziki, uwe wa kiasili au wa kisasa kama vile Pop, rock, reggae, hip hop, jazz, country, electronic na aina nyingine za muziki. Kujaza maombi kwa mtandao ingia HAPA

Mwaka jana Tamasha lilikuwa na washiriki kama The CITY band na Afro-jazz artist Siphokazi (Afrika ya Kusini), Nkwali (Zimbabwe), Cie Art Dic (Togo), kundi la ngoma za kiasili Twekembe Performers (Uganda),  Third Hand Music band (Kenya),  Karakeeb(Misri). Na kutoka Tanzania washiriki walikuwemo pia Inafrika Band. Kwa kufwatilia maendeleo ya tamasha hili pita  official website , pia  Twitter.

Comments