MUSICIANS BOOTCAMP YAFANA SANA


Mwanzoni mwa mwezi  Mei Culture and  Development East Africa (CDEA) ilitoa tangazo la kualika wanamuziki katika kambi ya mafunzo waliiita  Musicians Boot Camp. Kambi hii iliwekwa katika hoteli ya kitalii ya Red Monkey iliyoko Jambiani Zanzibar. Wanamuziki 20 walichaguliwa kuhudhuria kambi hii wakiwa ni mchanganyiko wa wanamuziki waimbaji wapigaji wa ala za kisasa na kiasili na wasanii wa Hiphop. Katika kambi hiyo baadhi ya masomo waliyojifunza ni
Digital Strategy, ambapo wasanii walijifunza namna ya kuboresha ‘brands’ zao katika ulimwengu wa kifijitali. Darasa hili liliongozwa na Jude Clark, mwanzilishi wa Joose Digital. Pia kulikuweko na darasa dogo la matumizi yenye tija ya mitandao ya kijamii.  Yusuf Mahmoud, Mtendaji Mkuu wa Sauti za Busara aliongelea umuhimu wa kushiriki matamasha kwa wanamuziki wa Tanzania. John Kitime akatoa somo kuhusu Copyright, Copyleft na Creative Commons. Somo hili lilifuatiwa na somo kutoka kwa Bi Rebecca Mkurugenzi Mtendaji wa Nafasi Art Space, yeye aliongelea somo lililoitwa Digitization of heritage music. Kuingiza katika dijitali muziki wetu wa Urithi. Somo ambalo lilifuatiwa na somo kutoka kwa Profesa Mitchel Strumpf, Mkurugenzi wa Masomo wa Dhow Countries Music Academy, Zanzibar alipoongelea namna ya kutunza urithi wa muziki. Hatimae masomo yaliongezwa thamani na elimu kutoka kwa  Sam Jones wa(Soundthread), John Kagaruki wa (Eyecuemedia) and Philemon Noirret wa (crazy only/tropical sound studio Zanzibar, ambao walielezea mambo mbalimbali kuhusu kurekodi na kufanya maonyesho live na maadili yake. Hakika elimu hii ni muhimu kuwafikia wanamuziki wengi zaidi.
Picha za Jam Session baada ya masomo












 


 

Comments