DISKO LEO DARLIVE WA MBAGALA MSIKOSE

DISKO la kukata na shoka linatarajiwa kuunguruma Ijumaa hii ndani ya Darlive, Mbagala Zakheem, Dar es Salaam katika shamrashamra za kuikaribisha wikiendi, imefahamika.
Mratibu wa Darlive, Juma Mbizo alisemajijini Dar es Salaam jana kuwa, disko hilo linaporomoshwa na Dj mahiri na maarufu kutoka kwenye moja ya radio zinazofanya vyema hivi sasa hapa nchini.
Mbizo alisema kuwa, kama ilivyo ada kwa siku za Ijumaa, wanawake wote watapenya bure, huku wanaume wakidondosha mlangoni mchango kiduchu wa buku tano.
“Nawaomba wapenda burudani wote wa Kitongoji cha Mbagala na Wilaya nzima ya Temeke kwa ujumla, kuhudhuria kwa wingi kwenye disko hilo, ili kufaidi raha isiyo na kifani,” alisema Mbizo, kati ya wadau wakubwa wa muziki hapa nchini.

Comments