Ili kuwezesha kufika Dodoma na kuwakilisha mapendekezo
yaliyokusanywa na Mashirikisho, Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (TAMUNET),
waliwezesha idadi ya wasanii 12 kufika na kuishi Dodoma. Wasanii hao wakiwemo
viongozi toka Mashirikisho wameza kufika Dodoma na kuanza kazi mara moja ya
kukutana na Wabunge mbalimbali, na kufanya nao mikutano na mazungumzo ya papo
kwa popa na kwa kweli mapokezi yamekuwa ya hali ya juu yanayoleta tumaini kubwa
kwa wote waliofika huku. Wasanii
waliomo katika msafara huu muhimu kwa tasnia na Taifa ni
1.
Simon Mwakifwamba – Rais, Shirikisho la Filamu
(TAFF)
2.
John Kitime – Mwenyekiti, Tanzania Musicians
Network (TAMUNET)
3.
Bishop Hiluka – Katibu Mkuu, TAFF
4.
Yobnesh ‘Batuli’ Yusuph –Msanii/FilmProducer
5.
Samwel ‘Braton’ Mbwana –Tanzania Urban Music
Association (TUMA)/Music Producer
6.
Paul ‘P Funk’ Matthysse – Mwenyekiti, Tanzania
Producers Association/ Producer
7.
Kulwa ‘Dude’ Kikumba – Msanii/ Producer
8.
Abdul Salvador –Katibu Mkuu, Shirikisho la
Muziki Tanzania (TMF)
9.
Adrian Nyangamale – Rais, _Shirikisho la Sanaa
za Ufundi Tanzania
10. Mh.
Paulynus Raymond Mtendah – Mbunge Bunge la katiba
11. Yvonne
Cherie ‘Mona Lisa’ –Msanii
12. Seleman
Hamisi- Producer toka Dodoma
13. Ernest
Omalla – Mshauri wa TAFF na TAMUNET
Kamati haikuishia hapo kwani jioni Mheshimiwa Makonda aliiwezesha kundi hili kukutana
na wabunge wengine wakiwemo Mh.
Ahmed Salum, Mh. William Mgeja na Mh. Mpina Mbunge wa Kisesa.
Katika hali ya
kuonyesha kuwajali wasanii wabunge wa Dar es Salaam waliwafuata wasanii katika
Lodge waliofikia na kuwasikiliza lile ambalo walikuwa wakilitaka. Mheshimiwa
Idd Azan na Mh. Abbas Mtemvu waliwakilisha wabunge wa Dar es Salaam na kuwa na
saa nzima ya kuwasikiliza wasanii hawa katika malengo yao
mawili waliyotaka yaingie katika Katiba.
Comments