SIMON MWAKIFWAMBA NA JOHN KITIME WAKUTANA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA MADANSA


Simon Mwakifwamba Rais  wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) na
John Kitime Mwenyekiti wa Tanzania Musicians Network)(TMN) siku ya Jumatano walikuwa na kikao kirefu na viongozi wa juu wa Tanzania Dancers Association (TDA). Mkutano huo uliokuwa umepangwa na viongozi wa TDA ulikuwa na madhumuni ya kupata experience ya uongozi wa vyama kutoka kwa viongozi hawa ambao wamekuwa wakiongoza vyama kwa muda mrefu. Pamoja na mengine yaliyoongelewa lilikuweko swala kubwa la kuhakiki kuwa TDA wairudie Katiba yao na kuifanyia marekibisho makubwa. Jambo ambalo viongozi wa TDA waliona walipangie  ratiba na kupata msaada kutooka kwa viongozi hao wawili.
TDA ni chama kipya cha madansa ambacho kinashirikisha kila aina ya madansa, tayari kuna matawi ya Mkoa na  wilaya tatu za Dar es salaam.








Comments