LANGA KILEWO AFARIKI DUNIA

Msanii mwingine wa Hiphop Langa Kilewo ayelianza kujulikana katika kundi la Wakilisha akiwa na Witness na Shaa amefariki dunia mchana huu. Taarifa za Langa kuwa amelazwa hospitali zilianza kujulikana mapema leo katika blog kadhaa zenye kufuatilia wasanii, zikieleza kuwa kalazwa kwa tatizo la malaria. Langa ambae aliwahi kukiri hadharani kuwa ana tatizo kubwa la madawa ya kulevya na kutangaza kuwa ameachana na madawa hayo kutokana na matatizo yaliyokuwa yanamletea. Hivi  karibuni kama wiki mbili zilizopita, Langa  alikuwa akihojiwa katika kipindi cha Friday Night Live cha EATV akawa akimuongelea marehemu Ngwear na kumsifu sana kuwa alikuwa na roho safi, pia Langa alikuwa anaelezea mipango yake ya baadae baada ya kutoa video yake mpya aliyoifanya na P Funk na Fid Q iliyokuwa ikiitwa Rafiki wa kweli. Alikuwa akiongelea kukamilisha video zake nyingine mbili ili kutoa album mwishoni mwa mwaka. Hayatakuwa.
MUNGU AMLAZE LANGA KILEWO PEMA PEPONI

Comments