Mwanamama maarufu kwa jina la Iron Lady, Bi Asha Baraka ambaye kwa miaka mingi amekuwa katika biashara ya muziki ameanza kuandaa hatua nyingine ya katika tasnia hii kwa kuwa katika matayarisho makubwa ya studio kubwa mpya itakayokuwa na idara ya video na audio, na hivyo kuweza kurekodi muziki na kutengeneza filamu. Studio hiyo iliyoko maeneo ya Vijana Social Hall Kinondoni, italeta changa moto mpya kwa wadau wote wa muziki nchini. Nilipata bahati ya kuruhusiwa kuingia kwenye studio hiyo ambayo sehemu kubwa bado iko katika matayarisho
 |
Chumba cha 'sound engineer' |
 |
Asha Baraka akiwa nje ya studio yake mpya, pamoja nae ni meneja maarufu wa bendi Zonte |
 |
Chumba cha editing cha filamu |
Comments