Wasanii mbalimbali wa fani ya muziki wenye majina hapa Nchini, wamethibitisha kushiriki katika Tamasha la Twanga Pepeta (Twanga Festival 2011) litakalofanyika siku ya Jumapili ya tarehe 06-11-2011 katika viwanja vya Leaders vilivyopo maeneo ya Kinondoni. wasanii hao ni pamoja na Isha Mashauzi akiwa na kundi lake la Mashauzi Classic, Msondo Ngoma Music Band, Schengen Academy na Prince Dully Sykes.
aidha kuna wasanii wengi ambao bado ASET ipo katika mazungumzo nao ili wafanye shoo katika Tamasha hilo.
Tamasha hilo ambalo sehemu kubwa litahusisha uzinduzi wa albamu ya 11 ya Bendi ya African Stars "Twanga Pepeta" inayojulikana kwa jina la "Dunia Daraja". Albamu itakuwa na nyimbo sita ambazo ni "Dunia Daraja" yenyewe iliyotungwa na Charlz Baba, "Penzi la Shemeji" imetungwa na Prince Mwnjuma Muumini, "Mtoto wa Mwisho" imetungwa na Dogo Rama, Kiongozi wa Bendi Bi Luizer Mbutu yeye ametungw

wiki ijayo katika nia ya kujiandaa vilivyo na Tamasha ili kuwapa wapenzi wake burudani ya uhakika Twanga Pepeta inataraji kuingia kambini katika sehemu itakayotangazwa hapo baadae na kwa sasa wanafanya matayarisho ya awali katika mazoezi yanayoendelea katika ofisi za ASET zilizopo Kinondoni nyuma ya Ukumbi wa Mamngo Garden uliopo Kinondoni Jijini Dar es salaam.
Albamu mpya imeongezewa nguvu na ujio wa wanamuziki wapya walioshiriki kikamilifu katika utengenezaji na hatimaye kurekodi nyimbo 4 ambazo ni Penzi la Shemeji, Mtoto wa Mwisho, Dunia Daraja na umenivika umasikini. wanamuziki hao wapya ni Mwinjuma Muumini aliyetokea Bwagamoyo Sound, Venance Joseph, pia katokea Bwagamoyo Sound, Grayson Semsekwa na Khadija Mnoga waliotokea Extra Bongo, mpiga gitaa la Solo Selemani Shaibu aliyetokea Akudo Impact na jumanne Said aliyetokeakwenye Bendi ya Ellystone Angai.
HASSAN REHANI.
MRATIBU WA TAMASHA.
Comments