UNATAKA KUSHIRIKI TUZO ZA MUZIKI ZA AFRIMA?

-->
Watayarishaji wa tuzo za All Africa Music Awards (AFRIMA) wamezindua uandikishaji wa watakaowania tuzo za AFRIMA kwa mwaka 2016. Wanaotaka kushiriki katika tuzo hizi wanatakiwa wawe wametuma maombi ifikapo tarehe 30 July 2016. Hii ni mara ya tatu kwa tuzo hizo kutolewa na kuna ‘category’ mbalimbali zitakazoshindaniwa. Mwaka huu shughuli za utoaji wa tuzo hizo utafanyika nchini Gambia, baada ya kufanyika Nigeria kwa mara mbili zilizopita. Tuzo hizo zimekwisha pata baraka ya Umoja wa Afrika (AU) hasa baada ya Angela Martins, Mkuu wa Idara ya Utamaduni ya Umoja wa nchi za Kiafrika kutamka wakati wakati wa uzinduzi wa tuzo hizi kuwa umoja huo utaendelea kukuza mahusiano ya nchi mbalimbalikwa kutumia  tasnia ya ubunifu katika kazi za muziki, na  kwa kuunganisha shughuli hizi katika matamko ya Charter for African Cultural Renaissance, African Youth Charter  na AU Plan of Action on Cultural and creative industries. Mike Dada, Rais na Executive Producer wa AFRIMA, amewaomba wasanii, mameneja, maproducer, wenye record labels, na maajent kuwahi kuwasilisha maombi ya wasanii wao. Alionya kuwa hata msanii akiwa maarufu namna gani AFRMA haitapokea kazi zilizochelewa kuwasilishwa, na wala AFRIMA haitawafuata wasanii popote. Tarehe ya kuanza kuwapigia kura wasanii itakuwa tarehe 26 Agosti 2016, na AFRIMA Academy itaanza kupitisha majina tarehe 26 Septemba 2016, na shughuli ya kutafuta washindi itaisha tarehe 5 Novemba 2016.
Kwa mwaka jana tuzo hizi ziliwawezesha Diamond Platnumz, Charlote Dipanda kupata tuzo tatu kila mmoja, washindi wengine walikuwa Stanley Enow na Olamide Ukitaka kushiriki ingia hapa


Comments

Unknown said…
Asante sn tunapoelekea pazuri